6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii pamoja,+ karibu watu mia nne, akawaambia: “Je, niende kupiga vita juu ya Ramothi-gileadi, au nijiepushe?” Nao wakaanza kusema: “Panda uende,+ na Yehova atalitia jiji hilo mkononi mwa mfalme.”
31 Manabii wenyewe kwa kweli wanatoa unabii kwa uwongo;+ nao makuhani wanakandamiza kulingana na nguvu zao.+ Na watu wangu wamependa mambo yawe hivyo;+ nanyi mtafanya nini mwisho wake?”+
32 Ijapokuwa hawa wanajua vema kabisa amri ya uadilifu ya Mungu,+ kwamba wale wanaozoea kufanya mambo ya namna hiyo wanastahili kifo,+ wao wanaendelea kuyafanya na vilevile hukubaliana+ na wale wanaozoea kuyafanya.