5 Tazama! Utaliita taifa ambalo hulijui,+ na watu wa taifa ambao hawakukujua watakimbia wakija kwako,+ kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ na kwa ajili ya Mtakatifu wa Israeli,+ kwa sababu atakuwa amekurembesha.+
2 Na mataifa mengi hakika yatakwenda na kusema: “Njooni,+ twendeni juu kwenye mlima wa Yehova na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo;+ naye atatufundisha njia zake,+ nasi tutatembea katika mapito yake.”+ Kwa maana sheria itatoka katika Sayuni, na neno la Yehova katika Yerusalemu.+
7 “ ‘Nami nitayatikisa mataifa yote, navyo vitu vyenye kutamanika vya mataifa yote vitaingia;+ nami nitaijaza nyumba hii utukufu,’+ asema Yehova wa majeshi.
8 Sasa Andiko, likitangulia kuona kwamba Mungu atawatangaza watu wa mataifa kuwa waadilifu kutokana na imani, lilitangaza habari njema kimbele kwa Abrahamu, yaani: “Kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”+