Wagalatia
3 Enyi Wagalatia wasio na akili, ni nani huyo aliyewaleta chini ya uvutano mwovu,+ ninyi ambao machoni penu Yesu Kristo alionyeshwa waziwazi akiwa ametundikwa mtini?+ 2 Nataka kujifunza hili peke yake kutoka kwenu: Je, mlipokea roho+ kutokana na matendo ya sheria+ au kutokana na kusikia+ kwa njia ya imani? 3 Je, ninyi hamna akili kabisa? Baada ya kuanza katika roho,+ je, sasa mnamalizia katika mwili?+ 4 Je, mlipatwa na mateso mengi sana bila kusudi?+ Ikiwa kwa kweli ilikuwa bila kusudi lolote. 5 Kwa hiyo, yeye anayewapa ninyi roho+ na kufanya matendo yenye nguvu+ katikati yenu, je, yeye hufanya hivyo kutokana na matendo ya sheria au kutokana na kusikia kwa njia ya imani? 6 Kama vile Abrahamu “alivyokuwa na imani katika Yehova, na ikahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu.”+
7 Hapana shaka mnajua kwamba wale wanaoshikamana na imani+ ndio wale walio wana wa Abrahamu.+ 8 Sasa Andiko, likitangulia kuona kwamba Mungu atawatangaza watu wa mataifa kuwa waadilifu kutokana na imani, lilitangaza habari njema kimbele kwa Abrahamu, yaani: “Kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”+ 9 Kwa sababu hiyo wale wanaoshikamana na imani wanabarikiwa+ pamoja na Abrahamu mwaminifu.+
10 Kwa maana wote wanaotegemea matendo ya sheria wako chini ya laana; kwa maana imeandikwa: “Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha Sheria ili ayafanye.”+ 11 Tena, kwamba hakuna yeyote ambaye kwa njia ya sheria hutangazwa kuwa mwadilifu+ kwa Mungu ni wazi, kwa maana “mwadilifu ataishi kwa sababu ya imani.”+ 12 Sasa Sheria haishikamani na imani, bali “yeye anayezifanya ataishi kwa hizo.”+ 13 Kristo kwa kutununua+ alituachilia huru+ kutoka katika laana ya Sheria kwa yeye kuwa laana+ badala yetu, kwa sababu imeandikwa: “Amelaaniwa kila mtu aliyetundikwa juu ya mti.”+ 14 Kusudi lilikuwa kwamba baraka ya Abrahamu ije kupitia Yesu Kristo kwa ajili ya mataifa,+ ili tuipokee roho iliyoahidiwa+ kupitia imani yetu.+
15 Akina ndugu, nasema kwa njia ya mfano wa mwanadamu: Agano lililohalalishwa, ingawa ni la mwanadamu, hakuna yeyote anayelifuta au kuongeza jambo juu yake.+ 16 Sasa ahadi zilitolewa kwa Abrahamu+ na kwa uzao wake.+ Haisemi: “Na kwa wazao,” kana kwamba ni wengi wa namna hiyo, bali kana kwamba ni mmoja:+ “Na kwa uzao wako,”+ ambaye ni Kristo.+ 17 Zaidi, mimi nasema hivi: Kuhusu agano lililohalalishwa na Mungu+ hapo kwanza, Sheria ambayo imekuja kuwapo miaka 430+ baadaye hailitangui, ili kuifuta ahadi.+ 18 Kwa maana ikiwa urithi ni kutokana na sheria, hautokani tena na ahadi;+ lakini Mungu amempa huo Abrahamu kwa fadhili kupitia ahadi.+
19 Basi, kwa nini Sheria? Iliongezwa ili kufanya makosa yawe wazi,+ mpaka ufike uzao+ ambao ulikuwa umepewa ahadi; na ilipitishwa kupitia malaika+ kwa mkono wa mpatanishi.+ 20 Sasa hakuna mpatanishi mahali ambapo ni mtu mmoja tu anayehusika, lakini Mungu ni mmoja tu.+ 21 Kwa hiyo, je, Sheria inapinga ahadi za Mungu?+ Hilo na lisitendeke kamwe! Kwa maana kama ingalitolewa sheria inayoweza kutoa uhai,+ kwa kweli uadilifu ungalikuwa kwa njia ya sheria.+ 22 Lakini Andiko+ liliyafunga mambo yote pamoja katika kifungo cha dhambi,+ ili ahadi inayotokana na imani kumwelekea Yesu Kristo ipewe wale wanaoamini.+
23 Hata hivyo, kabla ya ile imani kufika,+ tulikuwa tukilindwa chini ya sheria,+ tukiwekwa pamoja kifungoni, tukiitazamia imani iliyokusudiwa kufunuliwa.+ 24 Kwa sababu hiyo Sheria imekuwa mtunzaji wetu kutuongoza kwa Kristo,+ ili tutangazwe kuwa waadilifu+ kutokana na imani. 25 Lakini sasa kwa kuwa imani imefika,+ sisi hatuko tena chini ya mtunzaji.+
26 Ninyi nyote, kwa kweli, ni wana+ wa Mungu kupitia imani yenu katika Kristo Yesu. 27 Kwa maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo+ mmemvaa Kristo.+ 28 Hakuna Myahudi wala Mgiriki,+ hakuna mtumwa wala mtu huru,+ hakuna mwanamume wala mwanamke;+ kwa maana ninyi nyote ni mtu mmoja katika muungano na Kristo Yesu.+ 29 Zaidi ya hayo, ikiwa ninyi ni wa Kristo, ninyi kwa kweli ni uzao wa Abrahamu,+ warithi kuhusiana na ahadi.+