10 Na wale hasa waliokombolewa na Yehova watarudi+ na kuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe;+ na kushangilia kutakuwa juu ya kichwa chao mpaka wakati usio na kipimo.+ Watafikia furaha na kushangilia, na huzuni na kuugua zitakimbia kabisa.+
14 aliyejitoa mwenyewe+ kwa ajili yetu ili atukomboe+ sisi kutoka katika kila namna ya uasi-sheria na kujisafishia+ mwenyewe watu walio wake kwa njia ya pekee,+ walio na bidii kwa ajili ya kazi njema.+
15 Basi ndiyo sababu yeye ni mpatanishi+ wa agano jipya, ili, kwa sababu kifo kimetokea kwa ajili ya wao kuachiliwa huru kwa fidia+ kutoka kwenye makosa chini ya lile agano la zamani,+ wale ambao wameitwa waipokee ahadi ya urithi unaodumu milele.+