35 Kwa hiyo endeleeni kukesha,+ kwa maana hamjui bwana wa nyumba anakuja wakati gani, kama ni wakati wa jioni au katikati ya usiku au anapowika jogoo au asubuhi na mapema;+
15 “Tazama! Ninakuja kama mwizi.+ Mwenye furaha ni yule anayekaa macho+ na kutunza mavazi yake ya nje, ili asipate kutembea akiwa uchi na watu waitazame aibu yake.”+