1 Petro
5 Kwa hiyo, ninawapa himizo hili wanaume wazee walio kati yenu, kwa kuwa mimi pia ni mwanamume mzee+ pamoja nao na shahidi+ wa mateso ya Kristo, mshiriki hata wa utukufu utakaofunuliwa:+ 2 Lichungeni+ kundi la Mungu+ lililo chini ya uangalizi wenu, si kwa kulazimishwa, bali kwa kupenda;+ wala si kwa kupenda pato lisilo la haki,+ bali kwa hamu; 3 wala si kama kwa kupiga ubwana+ juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu,+ bali kuwa vielelezo kwa kundi.+ 4 Na mchungaji mkuu+ akiisha kufunuliwa, mtapokea taji la utukufu+ lisiloweza kufifia.+
5 Vivyo hivyo, enyi vijana, jitiisheni+ kwa wanaume wazee. Lakini ninyi nyote jifungeni unyenyekevu wa akili kuelekeana ninyi wenyewe,+ kwa sababu Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.+
6 Kwa hiyo, jinyenyekezeni chini ya mkono wenye nguvu wa Mungu, ili awainue ninyi katika wakati unaofaa;+ 7 huku mkitupa mahangaiko+ yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.+ 8 Tunzeni akili zenu, iweni wenye kulinda.+ Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta kummeza mtu.+ 9 Lakini chukueni msimamo mkampinge yeye,+ mkiwa imara katika imani, mkijua kwamba mambo yaleyale kwa njia ya mateso yanatimizwa katika ushirika mzima wa ndugu zenu ulimwenguni.+ 10 Lakini, mkiisha kuteseka kitambo kidogo,+ Mungu wa fadhili zote zisizostahiliwa, aliyewaita ninyi kwenye utukufu wake wa milele+ katika muungano+ na Kristo, yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu, atawafanya ninyi kuwa imara,+ atawafanya ninyi kuwa wenye nguvu.+ 11 Kwake yeye na kuwe na nguvu+ milele. Amina.
12 Kupitia Silvano,+ ndugu mwaminifu, kama ninavyomhesabu yeye, nimewaandikia ninyi kwa maneno machache,+ ili kutoa kitia-moyo na ushahidi wa bidii kwamba hizi ndizo fadhili zisizostahiliwa za Mungu zilizo za kweli; katika hizo simameni imara.+ 13 Mwanamke aliye katika Babiloni,+ mchaguliwa kama ninyi, anawatumia ninyi salamu zake, na vilevile Marko+ mwanangu. 14 Salimianeni kwa busu ya upendo.+
Na muwe na amani ninyi nyote mlio katika muungano na Kristo.+