Kumbukumbu la Torati 15:7 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zako atakuwa maskini kati yako katika moja la majiji yako, katika nchi yako ambayo Yehova Mungu wako anakupa, usiufanye moyo wako kuwa mgumu wala kuufunga mkono wako kumwelekea ndugu yako aliye maskini.+ Methali 3:27 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 27 Usiwanyime watu mema wanayostahili,+ mkono wako ukiwa na uwezo wa kuyafanya.+ Methali 21:26 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 26 Ametamani kwa hamu siku nzima, lakini aliye mwadilifu anatoa wala hanyimi kamwe.+ Mathayo 5:42 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 42 Mpe yeye anayekuomba, wala usimpe kisogo yule anayetaka umkopeshe bila faida.+
7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zako atakuwa maskini kati yako katika moja la majiji yako, katika nchi yako ambayo Yehova Mungu wako anakupa, usiufanye moyo wako kuwa mgumu wala kuufunga mkono wako kumwelekea ndugu yako aliye maskini.+