Mwanzo 6:5 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 5 Basi Yehova akaona kuwa ubaya wa mwanadamu ulikuwa mwingi duniani na kila mwelekeo+ wa fikira za moyo wake ulikuwa mbaya tu wakati wote.+ Mathayo 9:4 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 4 Naye Yesu, akijua fikira zao,+ akasema: “Kwa nini mnafikiri mambo maovu mioyoni mwenu?+ Mathayo 13:15 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 15 Kwa maana moyo wa watu hawa umekuwa mgumu, nao wamesikia kwa masikio yao bila kuitikia, nao wamefunga macho yao; ili wasione kamwe kwa macho yao na kusikia kwa masikio yao na kuelewa maana kwa mioyo yao na kugeuka, nami niwaponye.’+ Luka 5:22 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 22 Lakini Yesu, akifahamu mawazo yao, akawajibu, akasema: “Ni nini mnachowaza mioyoni mwenu?+
5 Basi Yehova akaona kuwa ubaya wa mwanadamu ulikuwa mwingi duniani na kila mwelekeo+ wa fikira za moyo wake ulikuwa mbaya tu wakati wote.+
15 Kwa maana moyo wa watu hawa umekuwa mgumu, nao wamesikia kwa masikio yao bila kuitikia, nao wamefunga macho yao; ili wasione kamwe kwa macho yao na kusikia kwa masikio yao na kuelewa maana kwa mioyo yao na kugeuka, nami niwaponye.’+