30 Zaidi ya hayo, wale aliowaagiza kimbele+ hao ndio aliowaita+ pia; na wale aliowaita hao ndio aliowatangaza kuwa waadilifu+ pia. Mwishowe wale aliowatangaza kuwa waadilifu hao ndio aliowatukuza pia.+
12 Kwa maana wakati wa sasa tunaona kwa njia isiyo ya waziwazi kupitia kioo cha chuma,+ lakini wakati huo itakuwa uso kwa uso.+ Wakati wa sasa najua kwa sehemu tu, lakini wakati huo nitajua kwa usahihi kama vile ninavyojulikana kwa usahihi.+
2 Wapendwa, sasa sisi ni watoto wa Mungu,+ lakini bado haijafunuliwa jinsi tutakavyokuwa.+ Tunajua kwamba wakati wowote atakapofunuliwa+ tutakuwa kama yeye,+ kwa sababu tutamwona kama vile yeye alivyo.+