30 Ndipo ishara ya Mwana wa binadamu+ itakapoonekana mbinguni, ndipo makabila yote ya dunia yatakapojipiga-piga yenyewe kwa kuomboleza,+ nayo yatamwona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi.+
32 Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake,+ naye atawatenganisha watu,+ mmoja kutoka kwa mwenzake,+ kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
10 Kwa maana sisi sote lazima tufunuliwe mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo,+ ili kila mmoja apate thawabu yake kwa ajili ya mambo yaliyofanywa kupitia mwili, kulingana na mambo ambayo ametenda, kama ni mema au ni maovu.+
10 kwa ajili ya usimamizi+ wa mambo kwenye kikomo kamili cha nyakati+ zilizowekwa rasmi, yaani, kukusanya tena pamoja+ vitu vyote katika Kristo,+ vitu vilivyo mbinguni+ na vitu vilivyo duniani.+ Ndiyo, katika yeye,
16 kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni+ akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu+ na kwa tarumbeta+ ya Mungu, na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza.+