Zaburi 149 Msifuni Yah!+Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+Sifa yake katika kutaniko la washikamanifu.+ 2 Israeli na ashangilie katika Mtengenezaji Mkuu wake,+Wana wa Sayuni—na wamshangilie Mfalme wao.+ 3 Na walisifu jina lake kwa kucheza dansi.+Na wampigie muziki kwa tari na kinubi.+ 4 Kwa maana Yehova anawafurahia watu wake.+Anawarembesha wapole kwa wokovu.+ 5 Washikamanifu na washangilie katika utukufu;Na wapige vigelegele kwa shangwe vitandani mwao.+ 6 Nyimbo zinazomsifu sana Mungu na ziwe kooni mwao,+Na upanga wenye makali kuwili uwe mkononi mwao,+ 7 Ili kutekeleza kisasi juu ya mataifa,+Kuvikemea vikundi vya mataifa,+ 8 Ili kuwafunga wafalme wao kwa minyororo+Na watu wao waliotukuzwa kwa pingu za chuma, 9 Ili kutekeleza juu yao uamuzi wa hukumu ulioandikwa.+Fahari ya namna hiyo ni ya washikamanifu wake wote.+Msifuni Yah!+