Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+
63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+
Nafsi yangu ina kiu kwa ajili yako.+
Mwili wangu umezimia kwa kukutamani wewe.
Katika nchi iliyokauka na kuchoka, ambapo hakuna maji.+
2 Hivyo nimekuona katika mahali patakatifu,+
Kwa kuona nguvu zako na utukufu wako.+
3 Kwa sababu fadhili zako zenye upendo ni bora kuliko uzima,+
Midomo yangu mwenyewe itakusifu.+
4 Kwa hiyo nitakusifu muda wote wa maisha yangu;+
Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.+
5 Nafsi yangu imeshiba sehemu bora, naam, mafuta,+
Na kwa midomo yenye vigelegele vya shangwe kinywa changu hutoa sifa.+
6 Wakati ninapokukumbuka kitandani mwangu,+
Wakati wa makesha ya usiku natafakari juu yako.+
7 Kwa maana umenisaidia,+
Na katika kivuli cha mabawa yako napiga vigelegele kwa shangwe.+
8 Nafsi yangu imekufuata karibu-karibu;+
Mkono wako wa kuume unanishika sana.+
9 Nao wale wanaoendelea kuitafuta nafsi yangu ili waiharibu,+
Wataingia katika sehemu za chini kabisa za dunia.+
10 Watatiwa katika nguvu za upanga;+
Watakuwa fungu la mbweha.+
11 Naye mfalme mwenyewe atashangilia katika Mungu.+
Kila anayeapa kwa jina lake atajisifu,+
Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitazibwa.+