Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
64 Ee Mungu, uisikie sauti yangu katika hangaiko langu.+
Uulinde uhai wangu kutokana na hofu ya adui.+
2 Unifiche mbali na mazungumzo ya siri ya watenda-maovu,+
Mbali na fujo ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza,+
3 Ambao wamenoa ulimi wao kama upanga,+
Ambao wameulenga mshale wao, maneno machungu.+
4 Ili wampige mtu asiye na lawama wakiwa mahali palipofichika.+
Wanampiga ghafula wala hawaogopi.+
5 Wanashikilia maneno mabaya;+
Wanasema juu ya kuficha mitego.+
Wamesema: “Ni nani anayewaona?”+
6 Wanaendelea kutafuta mambo yasiyo ya uadilifu;+
Wameficha mbinu ya werevu iliyofikiriwa sana,+
Na upande wa ndani wa kila mmoja, naam, moyo wake, una kina kirefu.+
7 Lakini Mungu atawapiga ghafula kwa mshale.+
Wamepata majeraha,+
8 Nao wanasababisha mtu ajikwae.+
Lakini ulimi wao huwapinga wao wenyewe.+
Wote wanaowatazama watatikisa kichwa chao,+
9 Nao watu wote wa udongo wataogopa;+
Nao watatangaza utendaji wa Mungu.+
Nao hakika watakuwa na ufahamu katika kazi yake.+
10 Na mwadilifu atashangilia katika Yehova na kwa kweli atamkimbilia;+
Nao wote walio wanyoofu moyoni watajisifu.+