Kwa kiongozi wa Yeduthuni. Muziki wa Daudi.
62 Kwa kweli nafsi yangu inamngojea Mungu kwa kimya.+
Wokovu wangu unatoka kwake.+
2 Kwa kweli yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kilele changu salama;+
Sitatikiswa sana.+
3 Mtaendelea mpaka wakati gani kumshambulia mtu ambaye mngetaka kumuua?+
Ninyi nyote ni kama ukuta unaoinama, ukuta wa mawe ambao unasukumwa ndani.+
4 Kwa kweli wanatoa mashauri ili kumshawishi mtu avunje heshima yake;+
Wanafurahia uwongo.+
Wanabariki kwa kinywa chao, lakini ndani yao wanalaani.+ Sela.
5 Kwa kweli mngojee Mungu kwa kimya, Ee nafsi yangu,+
Kwa maana tumaini langu ni kutoka kwake.+
6 Kwa kweli yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kilele changu salama;+
Sitatikiswa.+
7 Wokovu wangu na utukufu wangu uko juu ya Mungu.+
Mwamba wangu wenye nguvu, kimbilio langu liko katika Mungu.+
8 Mtegemeeni nyakati zote.+
Mimineni moyo wenu mbele zake.+
Mungu ni kimbilio letu.+ Sela.
9 Kwa kweli wana wa mtu wa udongo ni pumzi,+
Wana wa wanadamu ni uwongo.+
Wanapowekwa juu ya mizani wote pamoja ni wepesi kuliko pumzi.+
10 Msitegemee upunjaji,+
Wala kuwa ubatili kwa sababu ya unyang’anyi mtupu.+
Mali ikiongezeka, msiiweke moyoni.+
11 Mungu amesema mara moja, mara mbili nimelisikia hili,+
Kwamba nguvu ni za Mungu.+
12 Pia fadhili zenye upendo ni zako, Ee Yehova,+
Kwa maana wewe mwenyewe humlipa kila mmoja kulingana na kazi yake.+