Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 6:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 jiangalie usije ukamsahau+ Yehova, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya watumwa.

  • Ayubu 31:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu,

      Au nimeiambia dhahabu, ‘Wewe ni tegemeo langu!’+

  • Zaburi 52:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Huyo ndiye mwanamume ambaye hamweki Mungu kuwa ngome yake,+

      Lakini anategemea wingi wa utajiri wake,+

      Ambaye hulindwa kutokana na shida anazoleta.+

  • Methali 11:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Vitu vyenye thamani havitakuwa na faida yoyote siku ya ghadhabu,+ lakini uadilifu utakomboa kutoka katika kifo.+

  • Methali 11:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Anayetegemea utajiri wake​​—​yeye mwenyewe ataanguka;+ lakini waadilifu watasitawi kama majani.+

  • Methali 23:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Je, umeukazia macho, nao si kitu?+ Kwa maana hakika huo hujifanyia mabawa kama yale ya tai na kuruka kuelekea mbinguni.+

  • Mathayo 6:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Acheni kujiwekea hazina+ duniani, ambako nondo na kutu hula, na ambako wezi huvunja na kuiba.

  • Mathayo 6:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana ama atamchukia mmoja na kumpenda yule mwingine,+ ama atashikamana na mmoja na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kutumikia Mungu na Utajiri.+

  • Marko 8:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Kwa kweli, mtu anapata faida gani ikiwa ataupata ulimwengu wote na kuipoteza nafsi yake?+

  • Luka 12:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ndipo akawaambia: “Endeleeni kufungua macho yenu na mjilinde na kila namna ya tamaa,+ kwa sababu hata wakati mtu ana vitu vingi uzima wake hautokani na vitu alivyo navyo.”+

  • 1 Timotheo 6:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Uwape maagizo wale walio matajiri+ katika mfumo wa mambo wa sasa wasitake makuu,+ na waweke tumaini lao, si katika utajiri usio hakika,+ bali katika Mungu, ambaye hutupa sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie;+

  • 1 Yohana 2:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 kwa sababu kila kitu kilicho katika ulimwengu+—tamaa ya mwili+ na tamaa ya macho+ na mtu kujionyesha mali yake maishani+—hakitokani na Baba, bali hutokana na ulimwengu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki