1 Yohana
2 Watoto wangu wadogo, ninawaandikia ninyi mambo haya ili msitende dhambi.+ Na bado, yeyote akitenda dhambi, tuna msaidizi+ kwa Baba, Yesu Kristo, mtu mwadilifu.+ 2 Na yeye ni dhabihu+ ya upatanisho+ kwa ajili ya dhambi zetu,+ lakini si kwa ajili ya zetu+ tu bali pia kwa ajili ya zile za ulimwengu wote.+ 3 Na kwa jambo hili tunajua kwamba tumemjua yeye, yaani, tukiendelea kuzishika amri zake.+ 4 Yeye anayesema: “Mimi nimemjua,”+ na bado hashiki amri zake,+ ni mwongo, na kweli haimo ndani ya mtu huyo.+ 5 Lakini yeyote anayeshika neno+ lake, kwa kweli katika mtu huyo upendo kwa Mungu umekamilishwa.+ Kwa hili tunajua kwamba sisi tumo katika muungano na yeye.+ 6 Yeye anayesema kwamba anakaa katika muungano+ na yeye yuko chini ya wajibu yeye mwenyewe pia kuendelea kutembea kama vile huyo alivyotembea.+
7 Wapendwa, ninawaandikia ninyi, si amri mpya, bali amri ya zamani+ ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo.+ Amri hii ya zamani ni neno ambalo mlisikia. 8 Tena, ninawaandikia ninyi amri mpya, uhakika ambao ni wa kweli kumhusu yeye na kuwahusu ninyi, kwa sababu giza+ linapitilia mbali na nuru+ ya kweli tayari inaangaza.
9 Yeye anayesema kwamba yumo katika nuru na bado anamchukia+ ndugu yake yumo katika giza hata hivi sasa.+ 10 Yeye anayempenda ndugu yake hukaa katika nuru,+ na hakuna lolote la kumkwaza.+ 11 Lakini yeye anayemchukia ndugu yake yumo katika giza+ na anatembea katika giza, naye hajui anakoenda,+ kwa sababu giza limeyapofusha macho yake.
12 Ninawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya jina lake.+ 13 Ninawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye wa tangu mwanzo.+ Ninawaandikia ninyi, vijana,+ kwa sababu mmemshinda yule mwovu.+ Ninawaandikia ninyi, watoto wachanga,+ kwa sababu mmemjua Baba.+ 14 Ninawaandikia ninyi, akina baba,+ kwa sababu mmemjua yeye aliye wa tangu mwanzo.+ Ninawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu ninyi ni wenye nguvu+ na neno la Mungu hukaa ndani yenu+ nanyi mmemshinda yule mwovu.+
15 Msiwe mkiupenda ulimwengu au vitu vilivyo katika ulimwengu.+ Yeyote akiupenda ulimwengu, kumpenda Baba hakumo ndani yake;+ 16 kwa sababu kila kitu kilicho katika ulimwengu+—tamaa ya mwili+ na tamaa ya macho+ na mtu kujionyesha mali yake maishani+—hakitokani na Baba, bali hutokana na ulimwengu.+ 17 Zaidi ya hayo, ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake,+ lakini yeye anayefanya mapenzi+ ya Mungu anadumu milele.+
18 Watoto wachanga, ni saa ya mwisho,+ na, kama vile ambavyo mmesikia kwamba mpinga-Kristo anakuja,+ hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi;+ uhakika ambao kutokana nao tunajua kwamba ni saa ya mwisho. 19 Wao waliondoka kwetu, lakini hawakuwa wa namna yetu;+ kwa maana ikiwa wangekuwa wa namna yetu, wangebaki pamoja na sisi.+ Lakini wao waliondoka ili ionyeshwe wazi kwamba si wote walio wa namna yetu.+ 20 Nanyi mmepata kutiwa mafuta kutoka kwa yule mtakatifu;+ ninyi nyote mna ujuzi.+ 21 Ninawaandikia ninyi, si kwa sababu hamjui kweli,+ bali kwa sababu mnaijua,+ na kwa sababu hakuna uwongo wowote unaotokana na kweli.+
22 Ni nani aliye mwongo kama si yule anayekana kwamba Yesu ndiye Kristo?+ Huyo ndiye mpinga-Kristo,+ yeye anayemkana Baba na Mwana.+ 23 Kila mtu anayemkana Mwana hana Baba pia.+ Yeye anayemkiri+ Mwana ana Baba pia.+ 24 Kwa habari yenu, acheni lile ambalo mmesikia tangu mwanzo likae ndani yenu.+ Ikiwa lile ambalo mmesikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi pia mtakaa katika muungano+ na Mwana na katika muungano na Baba.+ 25 Zaidi ya hayo, hili ndilo jambo lililoahidiwa ambalo yeye mwenyewe alituahidi, uzima wa milele.+
26 Mambo haya ninawaandikia ninyi juu ya wale ambao wanajaribu kuwapotosha ninyi.+ 27 Na kwa habari yenu, kule kutiwa mafuta+ ambako mlipokea kutoka kwake hukaa ndani yenu, nanyi hamhitaji yeyote awe akiwafundisha;+ lakini, kama vile kutiwa mafuta kutoka kwake kunavyowafundisha ninyi juu ya mambo yote,+ na ni kweli+ wala si uwongo, na kama vile kumewafundisha ninyi, kaeni katika muungano+ na yeye. 28 Kwa hiyo sasa, watoto wadogo,+ kaeni katika muungano+ na yeye, ili wakati atakapofunuliwa+ sisi tuwe na uhuru wa kusema+ na tusipate aibu kutoka kwake katika kuwapo+ kwake. 29 Mkijua kwamba yeye ni mwadilifu,+ mnajua kwamba kila mtu aliye na mazoea ya kufanya uadilifu amezaliwa kutokana naye.+