1 Yohana
Barua ya Kwanza ya Yohana
1 Kile kilichokuwa tangu mwanzo,+ ambacho tumesikia,+ ambacho tumeona kwa macho yetu,+ ambacho tumetazama+ kwa uangalifu na mikono yetu ikakigusa,+ kuhusu neno la uzima,+ 2 (ndiyo, uzima ulifunuliwa,+ na sisi tumeona na tunatoa ushahidi+ na kuwapa ninyi habari juu ya uzima wa milele+ ambao ulikuwa pamoja na Baba na ukafunuliwa kwetu,) 3 kile ambacho tumeona na kusikia tunawapa ninyi habari pia,+ ili ninyi pia muwe na ushirika pamoja na sisi.+ Zaidi ya hilo, huu ushirika+ wetu ni pamoja na Baba na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.+ 4 Na kwa hiyo tunaandika mambo haya ili shangwe yetu ijae kwa ukamili.+
5 Na huu ndio ujumbe ambao tumesikia kutoka kwake nasi tunawatangazia ninyi,+ kwamba Mungu ni nuru+ na hakuna giza kamwe katika muungano na yeye.+ 6 Kama tukisema: “Tuna ushirika pamoja na yeye,” na bado tunaendelea kutembea katika giza,+ tunasema uwongo nasi hatuzoei kutenda kweli.+ 7 Hata hivyo, ikiwa tunatembea katika nuru kama yeye mwenyewe alivyo katika nuru,+ tuna ushirika sisi kwa sisi,+ na damu+ ya Yesu Mwana wake hutusafisha+ kutoka katika dhambi yote.+
8 Kama tukisema: “Sisi hatuna dhambi yoyote,”+ tunajipotosha wenyewe+ na kweli haimo ndani yetu. 9 Tukiungama dhambi zetu,+ yeye ni mwaminifu na mwadilifu hata atusamehe dhambi zetu na kutusafisha ukosefu wote wa uadilifu.+ 10 Kama tukisema: “Sisi hatujatenda dhambi,” tunamfanya yeye kuwa mwongo, na neno lake halimo ndani yetu.+