Ayubu
7 Ikiwa hatua zangu zinageuka kutoka katika njia,+
Au moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu tu,+
Au kasoro yoyote imeshikamana na mikono yangu,+
9 Ikiwa moyo wangu umeshawishiwa kumwelekea mwanamke,+
Nami nikaendelea kuvizia+ katika mlango wa rafiki yangu,
10 Basi mke wangu na amsagie mwanamume mwingine,
Wanaume wengine na wainame juu yake.+
12 Kwa maana huo ni moto ambao ungeteketeza mpaka kwenye maangamizi,+
Na katikati ya mazao yangu yote ungetia mizizi.
13 Ikiwa nilikuwa nikikataa hukumu ya haki ya mtumwa wangu
Au ya kijakazi wangu katika kesi yao juu yangu,
14 Basi naweza kufanya nini wakati Mungu atakaposimama?
Na wakati atakapotoza hesabu, naweza kumjibu nini?+
15 Je, Yeye aliyenifanya mimi tumboni hakumfanya yeye,+
Na je, si yeye Mmoja tu aliyetufanya sisi katika tumbo la uzazi?
16 Ikiwa nilikuwa nikiwanyima watu wa hali ya chini mapendezi yao,+
Na kuyafanya macho ya mjane yaishiwe nguvu,+
18 (Kwa maana tangu ujana wangu alikua pamoja nami kana kwamba pamoja na baba,
Na kutoka tumboni mwa mama yangu niliendelea kumwongoza huyo mjane);
19 Ikiwa nilikuwa nikiona mtu yeyote akiangamia kwa kukosa vazi,+
Au kwamba maskini hakuwa na cha kujifunika;
20 Ikiwa viuno vyake havikunibariki,+
Wala hakujipasha moto kwa sufu+ iliyokatwa ya wana-kondoo wangu;
21 Ikiwa nilitikisa mkono wangu huku na huku juu ya mvulana asiye na baba,+
Wakati nilipokuwa nikiona msaada wangu unahitajiwa katika lango,+
22 Acha mfupa wa bega langu uanguke kutoka katika bega lake,
Na acha mkono wangu uvunjwe kutoka kwenye mfupa wake wa juu.
25 Ikiwa nilikuwa nikishangilia kwa sababu mali yangu ilikuwa nyingi,+
Na kwa sababu mkono wangu ulikuwa umepata vitu vingi sana;+
27 Na moyo wangu ukaanza kushawishiwa kisiri+
Na mkono wangu ukakibusu kinywa changu,
28 Hilo pia lingekuwa kosa la kufikiriwa na waamuzi,
Kwa maana ningekuwa nimemkana Mungu wa kweli aliye juu.
29 Ikiwa nilikuwa nikishangilia kuangamia kwa mtu anayenichukia vikali,+
Au kuchangamka kwa sababu uovu umempata—
31 Ikiwa watu wa hema langu hawakusema,
‘Ni nani anayeweza kutokeza mtu ambaye hakushibishwa na chakula chake?’+—
33 Ikiwa kama mtu wa udongo niliyafunika makosa yangu+
Kwa kuficha kosa langu katika mfuko wa shati langu—
34 Kwa kuwa nilikuwa nikishtuka kwa sababu ya umati mkubwa,
Au dharau la familia lilikuwa likinitia hofu
Nami nilikuwa nikikaa kimya, sikuwa nikiondoka nje ya mlango.
35 Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikiliza,+
Kwamba Mweza-Yote angenijibu+ kulingana na sahihi yangu!
Au kwamba mtu aliye na kesi juu yangu angeandika hati!
36 Hakika ningeibeba juu ya bega langu;
Ningeifunga kunizunguka kama taji la fahari.