Zaburi Wimbo wa Mipando. 129 “Kwa muda mrefu wa kutosha wamenionyesha uadui tangu ujana wangu,”+Israeli na aseme sasa,+ 2 “Kwa muda mrefu wa kutosha wamenionyesha uadui tangu ujana wangu;+Hata hivyo hawajanishinda.+ 3 Walimaji wamelima juu ya mgongo wangu;+Wameirefusha mitaro yao.” 4 Yehova ni mwadilifu.+Amezikata vipande-vipande kamba za waovu.+ 5 Wataona aibu na kurudi nyuma wenyewe,+Wale wote wanaochukia Sayuni.+ 6 Watakuwa kama majani mabichi ya paa,+Ambayo yamekauka kabla hayajang’olewa,+ 7 Ambayo mvunaji hajajaza mkono wake kwa hayo,+Wala kifua chake yeyote anayekusanya miganda. 8 Wala wanaopita karibu hawajasema:“Baraka ya Yehova na iwe juu yenu.+Tumewabariki ninyi katika jina la Yehova.”+