-
Waroma 9:10-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Lakini si wakati huo tu, bali pia Rebeka alipopata mimba ya mapacha kupitia yule mwanamume mmoja, Isaka babu yetu;+ 11 kwa maana walipokuwa bado hawajazaliwa wala kufanya jambo lolote jema au baya, ili kusudi la Mungu kuhusu kuchagua liendelee kutegemea, si matendo, bali Yule ambaye huita, 12 Rebeka aliambiwa: “Mkubwa atakuwa mtumwa wa mdogo.”+ 13 Kama ilivyoandikwa: “Nilimpenda Yakobo, lakini nikamchukia Esau.”+
-