23 Yehova akamwambia: “Mataifa mawili yamo tumboni mwako,+ na mataifa mawili yatatenganishwa kutoka ndani yako;+ na taifa moja litakuwa na nguvu kuliko lingine,+ na mkubwa atamtumikia mdogo.”+
26 Kisha ndugu yake akatoka na mkono wake ulikuwa umeshika kisigino cha Esau,+ kwa hiyo akampa jina Yakobo.*+ Isaka alikuwa na umri wa miaka 60 Rebeka alipowazaa.
29 Mataifa na yakutumikie, mataifa na yainame chini mbele yako. Uwe bwana juu ya ndugu zako, na wana wa mama yako na wainame chini mbele yako.+ Alaaniwe kila mtu anayekulaani, na abarikiwe kila mtu anayekubariki.”+
37 Lakini Isaka akamjibu Esau: “Tazama, nimemweka awe bwana juu yako,+ nami nimempa ndugu zake wote wawe watumishi wake, nami nimempa nafaka na divai mpya ili kumtegemeza.+ Mwanangu, ni nini kilichobaki ninachoweza kukufanyia?”