Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 12:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yehova akamwambia Abramu: “Ondoka katika nchi yako na kutoka kwa watu wako wa ukoo na nyumba ya baba yako uende katika nchi nitakayokuonyesha;+

  • Mwanzo 12:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nitawabariki wale wanaokubariki, nami nitawalaani wale wanaokulaani,+ na familia zote duniani hakika zitabarikiwa* kupitia kwako.”+

  • Mwanzo 28:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Basi Isaka akamwita Yakobo, akambariki na kumwamuru hivi: “Usioe mke kutoka kwa mabinti wa Kanaani.+

  • Mwanzo 28:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Mungu Mweza-Yote atakubariki na kukufanya uwe na wazao wengi na kuongezeka, nawe hakika utakuwa kusanyiko la mataifa.+

  • Mwanzo 31:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Ikiwa Mungu wa baba yangu,+ Mungu wa Abrahamu, Yule ambaye Isaka anamwogopa,*+ hangekuwa pamoja nami, sasa ungeniambia niende zangu mikono mitupu. Mungu ameyaona mateso yangu na kazi ngumu ya mikono yangu, na ndiyo sababu alikukaripia usiku wa kuamkia leo.”+

  • Ezekieli 25:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nchi ya Edomu imelipiza kisasi dhidi ya nyumba ya Yuda nayo imepata hatia kubwa kwa kulipiza kisasi dhidi yake;+ 13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuwaangamiza wanadamu na wanyama waliomo, nami nitaifanya kuwa ukiwa.+ Kuanzia Temani mpaka Dedani, watauawa kwa upanga.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki