Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 12:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yehova akamwambia Abramu: “Ondoka katika nchi yako na kutoka kwa watu wako wa ukoo na nyumba ya baba yako uende katika nchi nitakayokuonyesha;+ 2 Nitakufanya kuwa taifa kubwa, nami nitakubariki, nami nitalifanya jina lako liwe kuu, nawe utakuwa baraka.+

  • Mwanzo 15:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Baada ya hayo neno la Yehova likamjia Abramu katika maono, likisema: “Usiogope,+ Abramu. Mimi ni ngao yako.+ Thawabu yako itakuwa kubwa sana.”+

  • Mwanzo 15:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Ndipo akamtoa nje na kumwambia: “Tafadhali, tazama juu mbinguni uzihesabu nyota, ikiwa unaweza kuzihesabu.” Kisha akamwambia: “Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”*+

  • Mwanzo 46:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Kisha Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku na kumwambia: “Yakobo, Yakobo!” naye akajibu: “Mimi hapa!” 3 Akamwambia: “Mimi ndiye Mungu wa kweli, Mungu wa baba yako.+ Usiogope kushuka kwenda Misri, kwa maana huko nitakufanya uwe taifa kubwa.+

  • Kutoka 1:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Na Waisraeli* wakazaana na kuanza kuongezeka sana, nao wakazidi kuwa wengi na kuwa na nguvu isivyo kawaida, hivi kwamba wakajaa nchini.+

  • Hesabu 2:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Hao ndio Waisraeli walioandikishwa kulingana na koo zao;* watu wote walioandikishwa katika kambi hizo ili kuwa wanajeshi walikuwa 603,550.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki