Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 15:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Mawimbi makubwa yaliwafunika; wakazama vilindini kama jiwe.+

  • Kutoka 15:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Ulipuliza bahari kwa pumzi yako, ikawafunika;+

      Walizama kama madini ya risasi katika maji makuu.

  • Kumbukumbu la Torati 11:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Hawakuona ishara zake na matendo yake aliyotenda Misri kwa Farao mfalme wa Misri na kwa nchi yake yote;+ 4 wala mambo aliyoyatendea majeshi ya Misri, farasi wa Farao na magari yake ya vita, ambayo yalifunikwa na maji ya Bahari Nyekundu walipokuwa wakiwafuatia ninyi, na Yehova akawaangamiza milele.*+

  • Yoshua 24:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Nilipokuwa nikiwatoa mababu zenu Misri,+ mlifika baharini, Wamisri waliwafuatia wakiwa na magari ya vita na askari wapanda farasi mpaka kwenye Bahari Nyekundu.*+ 7 Na mababu zenu wakaanza kumlilia Yehova,+ basi akaweka giza kati yenu na Wamisri na kuileta bahari juu yao ikawafunika Wamisri,+ na mliona kwa macho yenu wenyewe mambo niliyoyafanya huko Misri.+ Kisha mkaishi nyikani kwa miaka mingi.*+

  • Nehemia 9:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kisha ukafanya ishara na miujiza dhidi ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa nchi yake,+ kwa maana ulijua waliwatendea kwa kimbelembele.+ Ukajijengea jina ambalo limedumu hadi leo hii.+ 11 Nawe ukaitenganisha bahari mbele yao, wakavuka bahari juu ya nchi kavu,+ na wale waliowafuatia ukawatupa ndani ya maji mengi kama vile jiwe linavyotupwa ndani ya bahari iliyochafuka.+

  • Zaburi 78:53
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 53 Aliwaongoza kwa usalama,

      Nao hawakuogopa;+

      Bahari iliwafunika maadui wao.+

  • Waebrania 11:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Kwa imani walipita katika Bahari Nyekundu kama kwenye nchi kavu,+ lakini Wamisri walipojaribu kupita wakamezwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki