-
Kumbukumbu la Torati 11:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Hawakuona ishara zake na matendo yake aliyotenda Misri kwa Farao mfalme wa Misri na kwa nchi yake yote;+ 4 wala mambo aliyoyatendea majeshi ya Misri, farasi wa Farao na magari yake ya vita, ambayo yalifunikwa na maji ya Bahari Nyekundu walipokuwa wakiwafuatia ninyi, na Yehova akawaangamiza milele.*+
-
-
Yoshua 24:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Nilipokuwa nikiwatoa mababu zenu Misri,+ mlifika baharini, Wamisri waliwafuatia wakiwa na magari ya vita na askari wapanda farasi mpaka kwenye Bahari Nyekundu.*+ 7 Na mababu zenu wakaanza kumlilia Yehova,+ basi akaweka giza kati yenu na Wamisri na kuileta bahari juu yao ikawafunika Wamisri,+ na mliona kwa macho yenu wenyewe mambo niliyoyafanya huko Misri.+ Kisha mkaishi nyikani kwa miaka mingi.*+
-
-
Nehemia 9:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kisha ukafanya ishara na miujiza dhidi ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa nchi yake,+ kwa maana ulijua waliwatendea kwa kimbelembele.+ Ukajijengea jina ambalo limedumu hadi leo hii.+ 11 Nawe ukaitenganisha bahari mbele yao, wakavuka bahari juu ya nchi kavu,+ na wale waliowafuatia ukawatupa ndani ya maji mengi kama vile jiwe linavyotupwa ndani ya bahari iliyochafuka.+
-