Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 39:7-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Sasa baada ya hayo, mke wa bwana wake akaanza kumtupia jicho Yosefu na kumwambia: “Lala nami.” 8 Lakini akakataa na kumwambia mke wa bwana wake: “Tazama, bwana wangu hajui vitu nilivyo navyo nyumbani, naye ameniweka kuwa msimamizi wa vitu vyake vyote. 9 Hakuna yeyote aliye mkuu zaidi yangu katika nyumba hii, naye hajanikataza kitu chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe ni mke wake. Basi ninawezaje kufanya uovu huu mkubwa na kwa kweli nimtendee Mungu dhambi?”+

  • Kumbukumbu la Torati 5:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “‘Wala usifanye uzinzi.+

  • Methali 6:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Mtu yeyote anayefanya uzinzi na mwanamke hana busara;*

      Yule anayefanya hivyo anajiangamiza mwenyewe.+

  • Mathayo 5:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 “Mlisikia kwamba ilisemwa: ‘Usifanye uzinzi.’+ 28 Lakini ninawaambia kila mtu anayeendelea kumtazama mwanamke+ na kumtamani tayari amefanya uzinzi naye moyoni+ mwake.

  • Waroma 13:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Kwa maana sheria zinazosema, “Usifanye uzinzi,+ usiue,+ usiibe,+ usitamani,”+ na amri nyingine yoyote iliyopo, zimejumlishwa katika maneno haya: “Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”+

  • 1 Wakorintho 6:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Ukimbieni uasherati!*+ Dhambi nyingine yoyote ambayo huenda mtu akafanya iko nje ya mwili wake, lakini yeyote aliye na mazoea ya kufanya uasherati anautendea dhambi mwili wake mwenyewe.+

  • Waebrania 13:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kisiwe na unajisi,+ kwa maana Mungu atawahukumu waasherati* na wazinzi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki