Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 6:23-27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 “Mwambie hivi Haruni na wanawe: ‘Hivi ndivyo mtakavyowabariki+ Waisraeli. Waambieni:

      24 “Yehova na awabariki+ na kuwalinda.

      25 Yehova na awaangazie nuru ya uso wake,+ na kuwapa kibali chake.

      26 Yehova na ainue uso wake kuwaelekea na kuwapa amani.”’+

      27 Ni lazima waliweke jina langu juu ya Waisraeli,+ ili niwabariki Waisraeli.”+

  • Kumbukumbu la Torati 10:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “Wakati huo Yehova aliliteua kabila la Lawi+ ili libebe sanduku la agano la Yehova,+ lisimame mbele za Yehova ili kumhudumia, na kubariki katika jina lake,+ kama linavyofanya mpaka leo.

  • Kumbukumbu la Torati 21:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Nao makuhani, Walawi, watakuja kwa sababu Yehova Mungu wenu amewachagua wamhudumie,+ watangaze baraka katika jina la Yehova.+ Watatangaza jinsi kila mzozo unaohusisha ukatili unavyopaswa kusuluhishwa.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 23:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Wana wa Amramu walikuwa Haruni+ na Musa.+ Lakini Haruni alitengwa kando daima+ ili atakase Patakatifu Zaidi, yeye na wanawe, ili watoe dhabihu mbele za Yehova, wamhudumie, na kutangaza baraka katika jina lake sikuzote.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki