-
Mambo ya Walawi 3:3-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Atatoa sehemu ya dhabihu hiyo ya ushirika kuwa dhabihu kwa Yehova+ inayochomwa kwa moto, yaani, mafuta+ yanayofunika matumbo, naam, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo, 4 na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yaliyo karibu na kiuno. Ataondoa pia figo pamoja na mafuta yaliyo juu ya ini.+ 5 Wana wa Haruni watateketeza vitu hivyo kwenye madhabahu juu ya dhabihu ya kuteketezwa iliyo kwenye kuni zinazowaka moto ili vifuke moshi;+ ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+
-
-
Mambo ya Walawi 7:29-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 “Waambie Waisraeli, ‘Mtu yeyote anayemletea Yehova dhabihu yake ya ushirika atamtolea Yehova sehemu ya dhabihu hiyo.+ 30 Ataleta mafuta+ pamoja na kidari kwa mikono yake mwenyewe ili vitu hivyo viwe dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto, naye atavitikisa kwenda mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa+ mbele za Yehova. 31 Kuhani atayateketeza mafuta hayo kwenye madhabahu ili yafuke moshi,+ lakini kidari kitakuwa cha Haruni na wanawe.+
-