-
Mambo ya Walawi 12:7, 8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Kuhani atatoa dhabihu hizo mbele za Yehova ili kufunika dhambi ya mwanamke huyo, kisha atakuwa safi kutokana na damu yake. Hiyo ndiyo sheria kuhusu mwanamke anayezaa mtoto wa kiume au wa kike. 8 Lakini ikiwa hawezi kuleta kondoo, basi anapaswa kuleta njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga,+ mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa na wa pili kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, naye kuhani atamtolea dhabihu hizo ili kufunika dhambi yake, kisha atakuwa safi.’”
-
-
Mambo ya Walawi 14:21, 22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 “Hata hivyo, ikiwa mtu huyo ni maskini na hawezi kupata vitu hivyo, basi ataleta mwanakondoo dume mmoja atolewe kuwa dhabihu ya hatia na toleo la kutikiswa, ili atoe dhabihu ya kufunika dhambi yake, pia ataleta sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini uliochanganywa na mafuta ili uwe toleo la nafaka, logi ya mafuta, 22 na njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga, kulingana na uwezo wake. Ndege mmoja atatolewa kuwa dhabihu ya dhambi na wa pili dhabihu ya kuteketezwa.+
-
-
Mambo ya Walawi 15:13-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 “‘Mtu aliyekuwa akitokwa na umajimaji akipona na kuwa safi, atangoja kwa siku saba ili atakaswe, na ni lazima afue mavazi yake na kuoga kwenye maji ya kijito, naye atakuwa safi.+ 14 Siku ya nane, anapaswa kuchukua njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga+ na kwenda mbele za Yehova, kwenye mlango wa hema la mkutano na kumpa kuhani ndege hao. 15 Kisha kuhani atamtoa ndege mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi na ndege wa pili kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa, naye kuhani atamtolea mtu huyo dhabihu ya kufunika dhambi yake mbele za Yehova ili awe safi kutokana na umajimaji wake.
-