15 Musa akamwambia baba mkwe wake: “Ni kwa sababu watu wanaendelea kuja kwangu kutafuta mwongozo kutoka kwa Mungu. 16 Wakiwa na kesi, wanaileta kwangu, nami lazima niamue kesi yao, na kuwajulisha maamuzi ya Mungu wa kweli na sheria zake.”+
11 Yehova aliongea na Musa uso kwa uso,+ kama mwanadamu anavyoongea na mwanadamu mwenzake. Musa aliporudi kambini, Yoshua+ mwana wa Nuni, aliyekuwa mhudumu na mtumishi wake,+ hakuondoka hemani.
11 Mwana huyo wa mwanamke Mwisraeli akaanza kulikufuru lile Jina* na kulitukana.+ Basi wakamleta kwa Musa.+ Kumbe mama yake alikuwa Shelomithi, binti ya Dibri wa kabila la Dani. 12 Kwa hiyo wakamtia kifungoni mpaka walipojulishwa uamuzi wa Yehova.+