Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 22:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Basi wazee wa Moabu na wazee wa Midiani wakachukua malipo ya uaguzi* na kwenda kumwona Balaamu,+ wakamwambia maneno ya Balaki.

  • Hesabu 25:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Waisraeli walipokuwa wakikaa Shitimu,+ watu walianza kufanya uasherati na mabinti wa Moabu.+ 2 Wanawake hao waliwaalika kwenye dhabihu za miungu yao,+ nao watu wakaanza kula na kuinamia miungu yao.+ 3 Kwa hiyo Waisraeli wakashiriki katika kumwabudu* Baali wa Peori,+ na hasira ya Yehova ikawaka dhidi yao.

  • Hesabu 25:17, 18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 “Wachokozeni Wamidiani na kuwaangamiza,+ 18 kwa sababu wamekuwa wakiwachokoza kwa hila zao kama ilivyokuwa kule Peori+ na pia kuhusiana na Kozbi binti ya mkuu wa Midiani, dada yao aliyeuawa+ wakati pigo lilipotokea kwa sababu ya mambo yaliyotokea Peori.”+

  • 1 Wakorintho 10:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Wala tusifanye uasherati,* kama baadhi yao walivyofanya uasherati,* na 23,000 kati yao wakaanguka kwa siku moja.+

  • Ufunuo 2:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 “‘Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako, kwamba unao hapo wale wanaofuata fundisho la Balaamu,+ aliyemfundisha Balaki+ kuweka kikwazo mbele ya wana wa Israeli, ili wale vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na kufanya uasherati.*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki