Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 27:1-7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Kisha mabinti wa Selofehadi,+ mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa koo za Manase mwana wa Yosefu, wakaja. Mabinti hao waliitwa Mala, Noa, Hogla, Milka, na Tirsa. 2 Wakasimama mbele ya Musa, kuhani Eleazari, mbele ya wakuu,+ na mbele ya Waisraeli wote kwenye mlango wa hema la mkutano, wakasema: 3 “Baba yetu alikufa nyikani, lakini hakuwa miongoni mwa kikundi kilichojiunga na Kora kumpinga Yehova,+ bali alikufa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe naye hakuwa na mtoto yeyote wa kiume. 4 Kwa nini jina la baba yetu lipotee kutoka katika ukoo wake kwa sababu hakuwa na mtoto wa kiume? Tupe urithi miongoni mwa ndugu za baba yetu.” 5 Kwa hiyo Musa akawasilisha kesi yao mbele za Yehova.+

      6 Basi Yehova akamwambia Musa hivi: 7 “Mabinti wa Selofehadi wanasema ukweli. Kwa vyovyote vile unapaswa kuwapa urithi miongoni mwa ndugu za baba yao na urithi wa baba yao.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki