21Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Waambie hivi wana wa Haruni, makuhani: ‘Mtu yeyote kati yenu asijichafue kwa kumgusa mtu aliyekufa* miongoni mwa watu wake.+
2 “Waamuru Waisraeli wamtoe nje ya kambi kila mtu mwenye ukoma+ na kila mtu anayetokwa na umajimaji+ na kila mtu aliyejichafua kwa kumgusa mtu aliyekufa.*+
9 Lakini mtu akifa ghafla kando yake+ na kuchafua nywele zake ambazo ni ishara ya kwamba amejitenga kwa ajili ya Mungu,* ni lazima anyoe kichwa chake+ siku anapothibitisha utakaso wake. Anapaswa kukinyoa siku ya saba.
6 Sasa watu fulani hawakuwa safi kwa sababu waligusa mtu aliyekufa,+ hivyo hawangeweza kuitayarisha dhabihu ya Pasaka siku hiyo. Kwa hiyo wakaenda kumwona Musa na Haruni siku hiyo,+
19 Nanyi mnapaswa kupiga kambi nje ya kambi kwa siku saba. Kila mtu miongoni mwenu ambaye amemuua mtu na kila mtu ambaye amemgusa mtu aliyeuawa+ anapaswa kujitakasa+ siku ya tatu na siku ya saba, ninyi na mateka wenu.