Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 20:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 “Usitoe ushahidi wa uwongo dhidi ya jirani yako.+

  • Kutoka 23:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 “Usieneze habari za uwongo.+ Usishirikiane na mtu mwovu kwa kutoa ushahidi utakaowadhuru wengine.+

  • Mambo ya Walawi 19:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 “‘Usizungukezunguke kati ya watu wako ukieneza uchongezi.+ Usihatarishe uhai wa* mwenzako.+ Mimi ni Yehova.

  • Kumbukumbu la Torati 19:16-19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Shahidi mwenye nia ya kumdhuru mwingine akitoa ushahidi dhidi ya mtu na kumshtaki kwa kosa fulani,+ 17 watu hao wawili wanaozozana watasimama mbele za Yehova, mbele ya makuhani na waamuzi watakaokuwa wakihudumu wakati huo.+ 18 Waamuzi watachunguza jambo hilo kikamili,+ na ikiwa mtu huyo ni shahidi wa uwongo na ameleta shtaka la uwongo dhidi ya ndugu yake, 19 mnapaswa kumtendea kama alivyopanga kumtendea ndugu yake kwa hila,+ nanyi lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.+

  • Methali 6:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova anachukia;

      Naam, vitu saba vinavyomchukiza:

  • Methali 6:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Shahidi wa uwongo anayesema uwongo kila anapopumua,+

      Na mtu yeyote anayepanda ugomvi miongoni mwa ndugu.+

  • Methali 19:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Shahidi anayesema uwongo hatakosa kuadhibiwa,+

      Na yule anayesema uwongo kila anapopumua hataponyoka.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki