-
Mambo ya Walawi 26:3-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 “‘Mkiendelea kufuata sheria zangu na kushika amri zangu na kuzitekeleza,+ 4 nitawaletea mvua katika majira yanayofaa,+ nayo nchi itazaa kwa wingi,+ na miti ya matunda itazaa matunda mengi. 5 Majira yenu ya kupura nafaka yataendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na wakati wa kuvuna zabibu utaendelea mpaka wakati wa kupanda; nanyi mtakula mkate na kushiba na kuishi kwa usalama katika nchi yenu.+ 6 Nitaleta amani nchini,+ nanyi mtalala na hakuna yeyote atakayewaogopesha;+ nami nitawaondoa nchini wanyama wote wakali wa mwituni, na hakuna mtu yeyote atakayewashambulia kwa upanga katika nchi yenu. 7 Nanyi hakika mtawakimbiza maadui wenu na kuwaua kwa upanga. 8 Watu watano kati yenu watawakimbiza maadui 100, na 100 watawakimbiza 10,000; mtawaua maadui wenu kwa upanga.+
9 “‘Nitawabariki* na kuwafanya mzaane na kuongezeka,+ nami nitatimiza agano nililofanya pamoja nanyi.+ 10 Wakati wa mavuno mtakuwa bado mnakula mavuno ya zamani ya mwaka uliotangulia, mtahitaji kuondoa mavuno hayo ya zamani ili mpate nafasi ya mavuno mapya. 11 Nami nitaweka hema langu la ibada kati yenu,+ nami sitawakataa. 12 Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu,+ nanyi mtakuwa watu wangu.+
-