-
Mambo ya Walawi 26:14-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 “‘Lakini msiponisikiliza au kushika amri hizo zote,+ 15 mkikataa masharti yangu,+ mkichukia sheria zangu,* na kuvunja agano langu kwa kuacha kushika amri zangu zote,+ 16 basi, mimi nitawatendea mambo haya: nitawaadhibu kwa taabu, kwa kifua kikuu na homa kali, na kufanya macho yenu yadhoofike na uhai wenu uzorote.* Mtapanda mbegu zenu bure, kwa maana maadui wenu watazila.+ 17 Nitawakataa,* nanyi mtashindwa na maadui wenu;+ na wale wanaowachukia ninyi watawakanyaga-kanyaga,+ nanyi mtakimbia bila kukimbizwa na mtu.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 28:63Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
63 “Na kama Yehova alivyopendezwa wakati mmoja kuwafanikisha na kuwafanya mwongezeke, ndivyo Yehova atakavyopendezwa kuwaharibu na kuwaangamiza; nanyi mtang’olewa kutoka katika nchi mnayokaribia kuimiliki.
-