19 Yehova Mungu wenu atakapokuwa amewapumzisha kutokana na maadui wenu wote wanaowazunguka katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa kuwa urithi ili mwimiliki,+ mnapaswa kuwaangamiza kabisa Waamaleki ili wasikumbukwe tena chini ya mbingu.+ Msisahau jambo hilo.
20 Hata hivyo, Sauli akamwambia Samweli: “Lakini nimeitii sauti ya Yehova! Nimefanya kazi ambayo Yehova alinituma nifanye, nikamleta Agagi mfalme wa Waamaleki na kuwaangamiza Waamaleki.+
30Daudi na wanaume wake walipofika Siklagi+ siku ya tatu, Waamaleki+ walikuwa wamevamia upande wa kusini* na pia Siklagi, nao walikuwa wameshambulia Siklagi na kuliteketeza kwa moto.