-
1 Wafalme 9:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Watu wengine wote waliobaki miongoni mwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ ambao hawakuwa sehemu ya taifa la Israeli,+ 21 wazao wao waliobaki nchini, ambao Waisraeli walishindwa kuwaangamiza, Sulemani aliwaandikisha ili wafanye kazi ya kulazimishwa kama watumwa mpaka leo hii.+ 22 Lakini Sulemani hakumfanya Mwisraeli yeyote kuwa mtumwa,+ kwa sababu walikuwa mashujaa wake, watumishi, wakuu, makamanda wasaidizi, wakuu wa wale walioendesha magari yake ya vita na wapanda farasi wake.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 2:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Kisha Sulemani akawahesabu wanaume wote waliokuwa wakaaji wageni katika nchi ya Israeli,+ baada ya ile hesabu ya watu ambayo Daudi baba yake alikuwa amechukua,+ wakapatikana wanaume 153,600. 18 Kwa hiyo akawaweka watu 70,000 kati yao kuwa vibarua,* 80,000 kuwa wakataji wa mawe+ milimani, na 3,600 kuwa waangalizi wa kuhakikisha kwamba watu wanafanya kazi.+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 8:7-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Na watu wote waliobaki, yaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi+ ambao hawakuwa sehemu ya Waisraeli,+ 8 wazao wao waliobaki nchini—wale ambao Waisraeli hawakuwaangamiza+—Sulemani aliwaandikisha ili wafanye kazi ya kulazimishwa mpaka leo hii.+ 9 Lakini Sulemani hakumfanya Mwisraeli yeyote kuwa mtumwa wake,+ kwa sababu walikuwa mashujaa wake, wakuu wa makamanda wake wasaidizi, na wakuu wa waendeshaji wa magari yake ya vita na wapanda farasi wake.+
-