-
2 Mambo ya Nyakati 15:16-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Mfalme Asa alimwondoa hata Maaka+ nyanya yake kutoka katika cheo chake cha mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza sanamu chafu sana* kwa ajili ya ibada ya mti mtakatifu.*+ Asa akaikatakata sanamu hiyo chafu sana, akaipondaponda na kuiteketeza katika Bonde la Kidroni.+ 17 Lakini mahali pa juu hapakuondolewa+ Israeli.+ Hata hivyo, moyo wa Asa ulikuwa kamili* maisha yake yote.*+ 18 Naye alileta katika nyumba ya Mungu wa kweli vitu ambavyo yeye na baba yake walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu—fedha, dhahabu, na vyombo mbalimbali.+
-