-
2 Mambo ya Nyakati 20:35-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Baada ya hayo Mfalme Yehoshafati wa Yuda akaungana na Mfalme Ahazia wa Israeli, aliyetenda uovu.+ 36 Kwa hiyo akashirikiana naye katika kutengeneza meli za kwenda Tarshishi,+ walizitengenezea kule Esion-geberi.+ 37 Hata hivyo, Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha alitoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akisema: “Kwa sababu umeungana na Ahazia, Yehova ataharibu kazi zako.”+ Basi meli hizo zikavunjika,+ kwa hiyo hazikuweza kwenda Tarshishi.
-