-
Yeremia 26:20, 21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 “Na kulikuwa na mtu mwingine aliyetabiri katika jina la Yehova, Uriya mwana wa Shemaya kutoka Kiriath-yearimu,+ aliyetabiri dhidi ya jiji hili na dhidi ya nchi hii kwa maneno kama ya Yeremia. 21 Mfalme Yehoyakimu+ na wanaume wake wote hodari na wakuu wote wakayasikia maneno yake, na mfalme alitaka kumuua.+ Uriya aliposikia jambo hilo, mara moja akaogopa na kukimbilia Misri.
-
-
Yeremia 36:32Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine cha kukunjwa na kumpa Baruku mwana wa Neria, mwandishi,+ naye akaandika maneno yote aliyoambiwa na Yeremia ambayo yalikuwa katika kile kitabu cha kukunjwa ambacho Mfalme Yehoyakimu wa Yuda alikuwa amekiteketeza motoni.+ Na maneno mengine mengi kama hayo yakaongezwa.
-