-
1 Wafalme 3:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 nitafanya uliloomba.+ Nitakupa moyo wenye hekima na uelewaji,+ hivi kwamba kama vile ambavyo hajawahi kamwe kuwapo mtu mwingine kama wewe kabla yako, hatawahi kamwe kuwapo mtu mwingine kama wewe baada yako.+ 13 Isitoshe, nitakupa vitu ambavyo hukuomba,+ utajiri na utukufu,+ hivi kwamba hatakuwapo mfalme mwingine kama wewe katika maisha yako yote.*+
-
-
1 Wafalme 10:23-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Kwa hiyo Mfalme Sulemani alikuwa na utajiri+ mwingi zaidi na hekima+ kuliko wafalme wengine wote duniani. 24 Na watu wote duniani walitaka kukutana na* Sulemani ili wasikie hekima yake ambayo Mungu alikuwa ameweka moyoni mwake.+ 25 Kila mmoja wao alileta zawadi—vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, mavazi, silaha, mafuta ya zeri, farasi, na nyumbu—na walifanya hivyo mwaka baada ya mwaka.
-