-
1 Wafalme 12:1-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Rehoboamu alienda Shekemu, kwa maana Waisraeli wote walikuwa wamekuja Shekemu+ kumfanya kuwa mfalme.+ 2 Mara tu Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia habari hizo (bado alikuwa akiishi Misri kwa sababu alikuwa amemkimbia Mfalme Sulemani),+ 3 wakawatuma watu waende kumwita. Kisha Yeroboamu na Waisraeli wote wakaja kwa Rehoboamu na kumwambia hivi: 4 “Baba yako aliifanya nira yetu kuwa nzito.+ Lakini ukiufanya utumishi mzito wa baba yako kuwa mwepesi zaidi na kupunguza nira nzito* aliyotutwika, tutakutumikia.”
-