Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 7:51
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 51 Kwa hiyo Mfalme Sulemani akakamilisha kazi yote aliyopaswa kufanya kwa ajili ya nyumba ya Yehova. Kisha Sulemani akaingiza ndani vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa amevifanya kuwa vitakatifu,+ naye akaweka fedha, dhahabu, na vitu hivyo katika hazina za nyumba ya Yehova.+

  • 1 Wafalme 15:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Ndipo Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imebaki katika hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya* mfalme na kuwapa watumishi wake. Kisha Mfalme Asa akawatuma kwa Ben-hadadi mwana wa Tabrimoni mwana wa Hezioni, mfalme wa Siria,+ aliyekuwa akiishi Damasko, akamwambia:

  • 2 Wafalme 24:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Mfalme Yehoyakini wa Yuda akatoka nje kwenda kukutana na mfalme wa Babiloni,+ akiwa pamoja na mama yake, watumishi wake, wakuu wake, na maofisa wa makao yake;+ na mfalme wa Babiloni akamchukua mateka katika mwaka wa nane wa utawala wake.+ 13 Kisha akachukua hazina zote za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme.*+ Alivikata vipandevipande vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Sulemani mfalme wa Israeli alitengeneza katika hekalu la Yehova.+ Hilo lilitendeka kama Yehova alivyokuwa ametabiri.

  • 2 Wafalme 25:13-15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Pia Wakaldayo walivunja vipandevipande nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na magari+ na Bahari ya shaba,+ vitu vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova, nao wakaipeleka shaba hiyo Babiloni.+ 14 Walichukua pia ndoo za kuondolea majivu, sepetu, mikasi ya kukatia tambi za taa, vikombe, na vyombo vyote vya shaba vilivyotumiwa katika utumishi wa hekaluni. 15 Mkuu wa walinzi alichukua vyetezo na mabakuli yaliyotengenezwa kwa dhahabu+ na fedha halisi.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 12:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Basi Mfalme Shishaki wa Misri akashambulia Yerusalemu. Akachukua hazina za nyumba ya Yehova+ na hazina za nyumba ya* mfalme. Alichukua kila kitu, kutia ndani ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki