Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 7:15-22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Alitengeneza nguzo mbili kwa kutumia shaba iliyoyeyushwa;+ kila nguzo ilikuwa na urefu wa mikono 18, na kila moja ya nguzo hizo mbili ingeweza kuzungukwa kwa kamba yenye urefu wa mikono 12.*+ 16 Naye alitumia shaba iliyoyeyushwa kutengeneza vifuniko viwili ambavyo vingewekwa juu ya nguzo hizo. Kifuniko kimoja kilikuwa na urefu wa mikono mitano, na kingine kilikuwa na urefu wa mikono mitano. 17 Kifuniko cha kila nguzo kilikuwa na wavu uliofumwa wa minyororo;+ nguzo moja ilikuwa na nyavu saba na nguzo nyingine nyavu saba. 18 Naye alitengeneza safu mbili za makomamanga kuzunguka wavu uliofunika vifuniko vilivyokuwa juu ya nguzo; alifanya hivyo kwa kila nguzo. 19 Vifuniko vilivyokuwa juu ya nguzo za ukumbi vilikuwa na umbo la yungiyungi, na urefu wake ulikuwa mikono minne. 20 Vifuniko hivyo vilikuwa juu ya zile nguzo mbili, juu tu ya sehemu ya mviringo iliyoungana na zile nyavu; na kulikuwa na safu za makomamanga 200 kuzunguka kila kifuniko cha nguzo.+

      21 Alisimamisha nguzo za ukumbi wa hekalu.*+ Alisimamisha nguzo ya kulia* na kuiita Yakini,* kisha akasimamisha nguzo ya kushoto* na kuiita Boazi.*+ 22 Sehemu ya juu ya nguzo hizo ilikuwa na umbo la yungiyungi. Basi kazi ya kutengeneza nguzo ikakamilika.

  • 2 Wafalme 25:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa mikono 18,*+ na kifuniko chake kilikuwa cha shaba; na urefu wa kifuniko hicho ulikuwa mikono mitatu, na wavu pamoja na makomamanga yote yaliyozunguka kifuniko yalitengenezwa kwa shaba.+ Nguzo ya pili pamoja na wavu wake ilifanana na ya kwanza.

  • 2 Mambo ya Nyakati 4:11-13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Hiramu alitengeneza pia ndoo za kuondolea majivu, pia sepetu, na mabakuli.+

      Basi Hiramu akamaliza kazi yote aliyomfanyia Mfalme Sulemani kuhusiana na nyumba ya Mungu wa kweli:+ 12 zile nguzo mbili+ na vifuniko vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; na nyavu mbili+ za kufunika vifuniko hivyo viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; 13 yale makomamanga 400+ kwa ajili ya zile nyavu mbili, safu mbili za makomamanga kwa ajili ya kila wavu, ili kufunika vile vifuniko viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya zile nguzo;+

  • Yeremia 52:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Na kifuniko cha nguzo kilikuwa cha shaba; na urefu wa kila kifuniko ulikuwa mikono mitano;+ na wavu pamoja na makomamanga yote yaliyozunguka kifuniko hicho yalitengenezwa kwa shaba. Nguzo ya pili ilifanana na nguzo ya kwanza, pia yale makomamanga. 23 Kulikuwa na makomamanga 96 kandokando; jumla, kulikuwa na makomamanga 100 kuzunguka ule wavu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki