-
Nehemia 10:38, 39Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
38 Na kuhani, mwana wa Haruni, anapaswa kuwa pamoja na Walawi wanapokusanya sehemu ya kumi; Walawi nao wanapaswa kuleta sehemu ya kumi ya ile sehemu ya kumi katika nyumba ya Mungu wetu,+ kwenye vyumba vya* ghala. 39 Kwa maana Waisraeli na Walawi wanapaswa kuleta mchango+ wa nafaka, divai mpya, na mafuta+ kwenye maghala,* ambamo mna vyombo vya mahali patakatifu, na pia walinzi wa malango, waimbaji, na makuhani wanaohudumu. Hatutaipuuza nyumba ya Mungu wetu.+
-
-
Nehemia 12:44Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
44 Siku hiyo wanaume waliwekwa ili kusimamia maghala+ ya michango,+ mazao ya kwanza,+ na sehemu za kumi.+ Kutoka katika mashamba ya majiji walipaswa kukusanya kwenye maghala hayo mafungu yaliyoamriwa na Sheria+ kwa ajili ya makuhani na Walawi,+ kwa maana kulikuwa na shangwe huko Yuda kwa sababu ya makuhani na Walawi waliokuwa wakihudumu.
-