-
Ezra 9:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Baada ya mambo hayo kufanywa, wakuu wakaja na kuniambia: “Watu wa Israeli na makuhani na Walawi hawajajitenga na watu wa mataifa ya nchi mbalimbali na mazoea yao yanayochukiza,+ ya Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wayebusi, Waamoni, Wamoabu, Wamisri,+ na Waamori.+ 2 Wamejichukulia baadhi ya mabinti wa mataifa hayo kuwa wake zao na kuwachukulia wana wao pia.+ Sasa wao, uzao mtakatifu,*+ wamechanganyika na watu wa mataifa ya nchi mbalimbali.+ Wakuu na watawala wasaidizi ndio wanaoongoza katika ukosefu huu wa uaminifu.”
-
-
Malaki 2:7, 8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Kwa maana midomo ya kuhani inapaswa kulinda ujuzi, na watu wanapaswa kutafuta sheria* kutoka kinywani mwake,+ kwa sababu yeye ni mjumbe wa Yehova wa majeshi.
8 “Lakini ninyi wenyewe mmegeuka na kuiacha njia. Mmewafanya wengi wajikwae kuhusiana na sheria.*+ Mmeliharibu agano la Lawi,”+ asema Yehova wa majeshi.
-