Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezra 5:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Pia, Mfalme Koreshi alitoa katika hekalu la Babiloni vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua hekaluni huko Yerusalemu, na kuvileta katika hekalu la Babiloni.+ Alivikabidhi kwa mtu aitwaye Sheshbazari,*+ ambaye Koreshi alimteua kuwa gavana.+

  • Ezra 5:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Ndipo Sheshbazari akaja, akaweka misingi ya nyumba ya Mungu,+ iliyo Yerusalemu; na tangu wakati huo mpaka leo inaendelea kujengwa lakini haijamalizika.’+

  • Hagai 1:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, katika mwezi wa sita, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova lilikuja kupitia nabii Hagai*+ kwa Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli, gavana wa Yuda, na kwa Yoshua mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, likisema:

  • Hagai 1:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Basi Yehova akaichochea roho+ ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, gavana wa Yuda,+ na roho ya Yoshua+ mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na roho ya watu wengine wote; nao wakaja na kuanza kujenga nyumba ya Yehova wa majeshi, Mungu wao.+

  • Hagai 2:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 “‘Siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘nitakuchukua, mtumishi wangu Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli,’+ asema Yehova, ‘nitakufanya kuwa kama pete ya muhuri, kwa sababu nimekuchagua wewe,’ asema Yehova wa majeshi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki