Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 16:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Utando huo wa umande ulipotoweka, kitu laini, kinachovunjikavunjika,+ kitu laini kama theluji, kilienea kwenye ardhi nyikani.

  • Kutoka 16:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Waisraeli walikula mana kwa miaka 40,+ mpaka walipofika katika nchi iliyokaliwa na watu.+ Walikula mana mpaka walipofika mpakani mwa nchi ya Kanaani.+

  • Kutoka 16:31, 32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Watu wa nyumba ya Israeli waliuita mkate huo “mana.”* Ulikuwa mweupe kama mbegu za mgiligilani, na ladha yake ilikuwa kama ya keki bapa zenye asali.+ 32 Kisha Musa akasema: “Yehova ameamuru hivi: ‘Jazeni mkate huo katika kipimo cha omeri ili uwe kitu kitakachohifadhiwa katika vizazi vyenu vyote,+ ili watoto wenu waone mkate niliowapa mle nyikani nilipokuwa nikiwatoa katika nchi ya Misri.’”

  • Hesabu 11:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa kweli, mana+ ilikuwa kama mbegu za giligilani,+ na ilionekana kama utomvu wa mbedola.

  • Kumbukumbu la Torati 8:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa hiyo aliwanyenyekeza na kuwaacha mkae njaa,+ naye akawalisha mana,+ ambayo ninyi wala baba zenu hamkuwa mmeijua, ili awafundishe kwamba mwanadamu haishi kwa mkate tu bali huishi kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.+

  • Yohana 6:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Mababu zetu walikula mana nyikani,+ kama ilivyoandikwa: ‘Aliwapa mkate kutoka mbinguni ili wale.’”+

  • 1 Wakorintho 10:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 na wote walibatizwa katika Musa kupitia wingu na bahari, 3 na wote walikula chakula kilekile cha kiroho+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki