-
Hesabu 14:2-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Waisraeli wote wakaanza kumnung’unikia Musa na Haruni,+ na wote wakawalalamikia wakisema: “Laiti tungalifia katika nchi ya Misri, au laiti tungalifia hapa nyikani! 3 Kwa nini Yehova anatuleta kwenye nchi hii ili tuuawe kwa upanga?+ Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka.+ Je, si afadhali turudi Misri?”+ 4 Hata waliambiana: “Na tuchague kiongozi, turudi Misri!”+
-
-
1 Wakorintho 10:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Wala tusifanye uasherati,* kama baadhi yao walivyofanya uasherati,* na 23,000 kati yao wakaanguka kwa siku moja.+ 9 Wala tusimjaribu Yehova,*+ kama baadhi yao walivyomjaribu, wakaangamizwa na nyoka.+ 10 Wala tusiwe wanung’unikaji,+ kama baadhi yao walivyonung’unika, wakaangamizwa na mwangamizaji.+
-