Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 53:utangulizi-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • Kwa kiongozi; katika mtindo wa Mahalathi.* Maskili.* Wa Daudi.

      53 Mpumbavu* husema moyoni mwake:

      “Hakuna Yehova.”+

      Matendo yao maovu yamepotoka na yanachukiza;

      Hakuna yeyote anayetenda mema.+

       2 Lakini Mungu anawatazama wanadamu kutoka mbinguni+

      Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+

       3 Wote wamekengeuka;

      Wote wamepotoka.

      Hakuna yeyote anayetenda mema,

      Hakuna hata mmoja.+

       4 Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa?

      Wanawala watu wangu kwa pupa kana kwamba wanakula mkate.

      Hawamwiti Yehova.+

       5 Lakini watajawa na hofu kubwa,

      Hofu ambayo hawajawahi kamwe kuwa nayo,*

      Kwa maana Mungu ataitawanya mifupa ya wale wanaowashambulia ninyi.*

      Mtawaaibisha, kwa maana Yehova amewakataa wao.

       6 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+

      Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,

      Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.

  • Waroma 3:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwanadamu mwadilifu, hakuna hata mmoja;+ 11 hakuna yeyote aliye na ufahamu; hakuna yeyote anayemtafuta Mungu. 12 Watu wote wamegeuka kando, wote wamekuwa wasiofaa kitu; hakuna yeyote anayetenda kwa fadhili, hakuna hata mmoja.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki